Monday, March 16, 2009

Tuesday, November 4, 2008

I have a dream imemkuwa kweli.

AND NOW I AND I WAITING FOR THE BLACK STAR LINER SHALL COME.

Friday, October 31, 2008

hatuaminiki hata kwa 5000.

wakati mwingine nabaki mdomo wazi na kujiuliza maswali mengi yasiyo na majibu ndio maana huwa naamini kuna WATU NA BIN ADAM.Tamaa ni kitu kibaya sana,unataka mabadiliko wakati mimi mwenyewe sijabadilika,unataka kukwapua wakati hutaki vyakwako kukwapuliwa.
5000 inakufanya kuto kuaminika na jamii?
kweli kuna watu na bin adamu.

tunaanza mwenzi hivi.

kulingana na mtazamo wako naomba mchango wako kulingana na hiyo picha.

Thursday, October 30, 2008

siku inakuja Afrika itaungana,siku inakuja waafrika wote waishio ughaibuni watarudi nyumbani

maneno yake Nabii Marcus Garvey
ndoto ambayo bado haijatimia lakini muda si mrefu maneno yake nabii Marcus Garvey yatatimia,itakuwa siku ya furaha sana pale tutakuwa ufukweni kuwapokea ndugu zetu kutoka ughaibuni,itakuwa siku ya furaha kwani tutawakaribisha nchi ya ahadi SHASHAMANE.
naamini katika nguvu na uwezo wa aliye hai Mfalme haile sellasi i atafanikisha Afrika iungane na kuwa kitu kimoja,naamini siku inakuja Afrika itakuwa na amani na upendo,naamini siku inakuja Afrika haitakuwa na maskini wala tajiri.bado naamini mimi na mimi unapenda sana.
Hivi naomba kuuliza,eti ni vigumu kusoma shahada ya udhamili hapa Afrika?au nauliza tena eti nivigumu kusoma katika mazingira ya hapa nyumbani mpaka uende kusoma nje?sasa nami nashangaa pake mzaliwa wa afrika anapokuja kutalii nchi yake.Eti ukijuwa lugha za kigeni kuliko lugha za nyumbani ni sifa ehhhh.

je unaikumbuka ijumaa nyeusi?

hivi vyombo vya habari vinavyo habarisha kuhusu vita vinahamasisha amani au mapambano?

Tuesday, October 28, 2008

lini Bara la Afrika litakaa kwa amani?




unasema unaamani?
unasema unakula kwa amani?
unalala kwa amani
wakati ndugu zetu wanatembea kutafuta amani.
congo iwe naamani,Afrika iwe na amani,watoto,wazee,kina mama hawana makosa.kama kweli mnataka kupigana,mngetafuta uwanja wenu wa mapambona nasio kuwahusisha ambao hawajui lolote.
swali,hivi hao waasi wanapata wapi silaa?nini kina cha vita huko congo?
amani bara la Afrika.